This is featured post 1 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgan1RFf60ForospUB-yYR1zLtop_M6KgLtKHuEaQZp5MSv6L1nJt6WpPaotUMk7WTPWiGfAzqD7ISb-knHwH3bRj9UNkkNyp-6_uR3yeOPCjkNEVvUEL6jgP9ZjWnz6CDLhis9I6kijPw/s1600/DSC_0000047.jpg)
This is featured post 2 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjFWH61LnGSFkBLf-F5yhz7h9xFL89UTicjHH3uZOeC_gyBUqFYbInlLl3We4DE9beL-hUggPrTB4NwfU-nQz6LzJfXWkE0JfcR9ypTdmDWxkL9SdJdawpZV5zAUABuu45uzuLnHbJZh7Y/s1600/DSC_0000087.jpg)
This is featured post 3 title
Replace these every slider sentences with your featured post descriptions.Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha - Premiumbloggertemplates.com.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEghvt4Bq6oMu2vQJ-875hyphenhyphenYTdrdlbEhB-KD2zs0ogMgya4k1FY9ZlEWzomzp6dRmAbiGyeWxqkW-KKpG7wIvoLqcMlW3MvcHNdpynK9AFYF-ZppzrbU6Y6E7twSJlZCWmq3N26cL1Modes/s1600/DSC_0000086.jpg)
Thursday, 7 April 2016
![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Ligi ya mabingwa barani ulaya imeendelea kwa michezo miwili ya robo fainali kuchezwa.
Wolfsburg wakiutumia vyema uwanja wao wa Volkswagen Arena, wamepata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Real Madrid.
Ricardo Rodriguez ndiye alianza kuipatia timu yake bao la kwanza kwa mkwaju wa penati baada ya Andre Schurrle kufanyiwa madhambi na Casemiro.
Katika dakika ya 18 Max Arnold akaongeza bao la pili na kuwazamisha kabisa vijana wa Zidane.
Nao Man City wakicheza ugenini huko nchini Ufaransa walikwenda sare ya kufunga kwa mabao 2-2, mabao ya Psg yalifungwa na mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic na Adrien Rabiot.
Huku mabao ya Man City yakifungwa na viungo Kevin De Bruyne na Fernandinho, mshambuliaji Zlatan Ibrahimovic alikosa mkwaju wa penati uliokolewa na kipa Joe Hart.![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Mamba mkubwa mla ng’ombe ameuawa katika jimbo la Florida nchini Marekani.
Mnyama huyo alikuwa na uzani wa kilo 360.
Mwindaji Lee Lightsey amesema mamba huyo wa ukubwa wa futi 15 (4.5m) ndiye mkubwa zaidi ambaye amekumbana naye katika kipindi cha miaka 18.
Baada ya kumuua, alihitaji trekta kumbeba.
Bw Lightsey alimgundua mnyama huyo akiwa na mwelekezi wa wawindaji Blake Godwin walipokuwa katika maeneo ya kumnyweshea mifugo maji Jumamosi.
Walimfyatulia risasi mamba huyo alipokuwa umbali wa mita sita kutoka kwao.
"Ingawa mnyama huyu ni mnene hivi, sijashangaa kwamba amekuwepo,” amesema Bw Lightsey.
- Je wajua siri ya Mamba usingizini?
- Mamba kulinda wafungwa hatari Indonesia
- Kwa Picha: Ndovu dhidi ya mamba
“Tumewapata wengi ambao wamekuwa wadogo kiasi tu kumshinda katika miaka 20 ambayo tumekuwa tukiwinda.
"Kilichotuvutia ni kwamba anaonekana amekuwa akiwala ng’ombe wetu, kwa sababu tulipata vipande vya nyama majini. Alikuwa dubwana lililostahili kuangamizwa.”
Bw Lightsey anasema mamba mkubwa zaidi ambaye amewahi kumuua alikuwa na urefu wa futi 13ft (4m).
Mamba wa Marekani hupatikana mashariki mwa Marekani katika majimbo ya Florida na Louisiana, kila jimbo likiwa na zaidi ya mamba milioni moja.
Eneo la kusini mwa Florida ndilo pekee ambalo mamba wa Marekani na mamba wa kawaida huishi kwa pamoja.
Bw Lightsey amesema anapanga kumhifadhi mamba huyo lakini nyama yake ataikabidhi kwa wahisani.![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Kiongozi wa mashtaka wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu na makosa ya jinai ICC yenye makao yake makuu nchini Uholanzi, bi Fatou Bensouda ameilaumu serikali ya Kenya kwa kuhujumu kesi dhidi ya watuhumiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka wa 2007 naibu rais William Ruto na mwandishi Joshua arap Sang.
Katika ujumbe wa video uliochapishwa kwenye mtandao wa Youtube bi Bensouda anasema kuwa mashdi wake walihongwa wengine wakatengwa baada ya kutishwa na kushinikizwa kujiondoa kama mashahidi.
''Tunasikita kuwa kutokana na shinikizo na hujuma dhidi ya mashahidi wetu kutoka kwa watu wenye uwezo mkubwa nchini Kenya, jopo la majaji wa mahakama ya kimataifa ya ICC lilishindwa kutoa hukumu kutokana na ushahidi halisi tulioyokuwa nayo.
Katika tukio hili, mashahidi 17 wa upande wa mashtaka waliokuwa wameahidi kutoa ushahidi dhidi ya watuhumiwa walijiondoa wakihofia maisha yao.
Yamkini walikuwa wanatishiwa maisha yao, wengine walitengwa na jamii
Licha ya serikali ya Kenya kuahidi kuwa ingeshirikiana na mahakama ya kimataifa ya ICC ukweli ni kwamba serikali ya Kenya haikutoa 100% ya ushirikiano na mahakama ya ICC.
Hii ilisababisha afisi ya kiongozi wa mashtaka kukosa ushahidi uliohitajika kuthibitisha tuhuma dhidi ya washukiwa wakuu.
Vizuizi tulivyowekewa na washirika wa watuhumiwa wakuu wa mauaji na makosa ya uhalifu wa kivita yaliyotokea punde baada ya uchaguzi wa mwaka wa 2007 ulisababisha tukashindwa kuwawajibisha wale waliosababisha ghasia hizo na hivyo tumeshindwa kuwapa haki wale wahanga wa ghasia hizo.'' Taarifa hiyo ya kiongozi wa mashtaka ilisema.
Bi Fatou Bensouda hata hivyo hakufa moyo anaiitaka serikali ya Kenya ichukue hatua kwa niaba ya wahanga wa machafuko hayo ya mwaka wa 2007 na kuwakamata mwandishi wa habari Walter Barasa, wakili Paul Gicheru na Philip Bett na kuwakabidhi kwa maafisa wa mahakama hiyo ya Uholanzi.
Watatu hao wanatafutwa na mahakama hiyo ya ICC kwa madai ya kutoa hongo kwa mashahidi na kwa kuwatishia mashahidi wa ICC hadi wakajiondoa.
Tayari vibali vya kukamatwa kwao vimeshatolewa.
Hapo jana jopo la majaji Olga Herrera Carbuccia, Chile Eboe-Osuji na Robert Fremr lilikubaliana na bi Bensouda kuwa mashahidi wengi walihongwa na kutishiwa maisha hadi wakajiondoa kufuatia shinikizo kubwa la kisiasa na hivyo wakawaondolea mashtaka naibu wa rais William Ruto na mwandishi habari Joshua arap Sang .![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Bunge la Ufaransa limeidhinisha sheria mpya, inayopinga biashara ngono
Hatua hiyo inadaiwa kwamba huenda ikaathiri maisha ya watu zaidi ya elfu thelathini ambao wanategemea shughuli za ngono katika kujipatia kipato ambao wengi wao ni raia wa kigeni.
Chini ya sheria hiyo mpya, watu watakaokutwa wakilipia huduma hiyo wataadhibiwa kwa kulipa dola 1,700.
Mmoja wa mbunge anayeunga mkono sheria hiyo ameitetea na kusema kuwa inalengo la kuhamasisha watu kujiondoa katika biashara hiyo.
Hata hivyo kundi dogo la makahaba waliandamana nje ya bunge wakipinga sheria hiyo kwa madai kuwa wapewe uhuru wa kujilinda wenyewe na si kukatazwa kufanya biashara hiyo.![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Rwanda na Tanzania zimeahidi kushirikiana zaidi kibiashara katika ukurasa mpya wa uhusiano baina ya mataifa hayo jirani.
Hayo yamewadia katika mkutano wa rais wa Rwanda Paul Kagame na mgeni wake rais wa Tanzania John Pombe Magufuli.
Marais hao wameyasema hayo leo mnamo mwanzo wa ziara ya rais Magufuli nchini Rwanda ambayo ndiyo ziara yake ya kwanza kuchaguliwa kwake mwaka uliopita.
Maneno ya undugu,urafiki ,uhusiano mwema na uhusiano imara yametamkwa sana na viongozi hawa,Rais Kagame akisisitiza ndio ndiyo msingi mkubwa wa kujenga nchi hizi mbili.
Ziara hiyo ya siku mbili inaangaliwa na wengi kama ya kufungua ukurasa mpya wa uhusiano kati ya nchi hizo mbili baada ya kipindi Fulani cha uhusiano baridi.
''Mnajua vyema kuwa mimi sipendi kusafiri, kwa sababu ninapenda kubana matumizi.
''Nimealikwa sehemu nyingi hata ulaya nimealikwa lakini bado sijaenda.
''Lakini nilipoalikwa na rais kagame mnaona nimeshafika hapa''
Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli mara tu baada ya uzinduzi wa daraja la Rusumo linalounganisha Tanzania na Rwanda ambalo amelizindua rasmi yeye na mwenyeji wake Rais wa Rwanda Paul Kagame.
''Nimefurahi kwa sababu nimekuja kufungua daraja la Rusumo.
''Hii ni Historia kubwa inayojengeka kati ya Tanzania na Rwanda''.
''Lakini nataka kuwahakikishia ndugu zangu wa Rwanda kuwa Tanzania itatoa ushirikiano mkubwa sana kwa nchi ya Rwanda'' alisema rais Magufuli.
Rais wa Rwanda Paul Kagame akihutubia hadhira hiyo alisema
''Tunataka amani,undugu urafiki na tunataka kufanya biashara ili kila mmoja wetu aweze kupata faida''
Ziara hii ya kwanza ya Rais Magufuli nje ya nchi yake inaangaliwa na wengi hapa Rwanda kama ya kuanza ukurasa mpya wa uhusiano kati ya nchi mbili.
Miaka ya nyuma uhusiano huo uliingiwa baridi baada ya Tanzania kuwatimua raia wa Kinyarwanda ,kitendo kilichowakasirisha viongozi wa Rwanda.Hayo yalifwatia kipindi kigumu cha uelewano mdogo baina ya nchi mbili kuhusu swala la mgogoro wa mashariki ya Congo.
Rwanda kama nchi isiyopakana na bahari kibiasha hutegemea sana bandari ya Dar es Salam na hivi karibuni Rais Kagame alimsifu mgeni wake na kuahidi kuiga mfano wake katika juhudi za kupambana na rushwa na ufisadi.
Rais Magufuli kesho ataungana na wananchi wa Rwanda katika maadhimisho ya miaka 22 ya kumbukumbu ya mauaji ya kimbari kabla ya kufanya mazungumzo na wandishi wa habari akiwa pamoja na Rais Paul Kagame.
Mshirikishe mwenzako Unavyoweza kumshirikisha mwenzako
Tuesday, 2 June 2015
![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Kilabu ya Manchester United inaamini iko katika nafasi nzuri ya kumsajili Dani Alves kutoka Barcelona iwapo kocha Louis Van Gaal anataka kumsajili beki huyo wa kulia.
Alves atakuwa hana mkataba mwishoni mwa msimu huu na Barcelona iko tayari kumwachilia beki huyo wa miaka 32 kuondoka baada ya mechi ya fainali ya vilabu bingwa Ulaya dhidi ya Juventus siku ya jumamosi mjini Berlin.
Klabu ya PSG pia inamuania Alvez ijapokuwa kocha wake Laurent Blanc anaamini mchezaji huyo bado anataka kusalia Barcelona.
Lakini maoni ya Old Trafford ni kwamba Alvez hangependelea kujiunga na PSG.
Van Gaal anapanga kumsajili beki wa kulia.Licha ya umri wake mkubwa ukosefu wa fedha za uhamisho zinamfanya mchezaji huyo kuwa muhimu.
Mchezaji huyo wa Brazil anapokea kitita cha pauni 120,000 kwa wiki, fedha ambazo United inaweza kuzilipa bila kutoa jasho.
![](http://1.bp.blogspot.com/-Kf6Dp9nzOV0/UYxS1vdihnI/AAAAAAAAJJI/2MTELq8IXbs/s000/date.png)
![](http://2.bp.blogspot.com/-KsISg7lKRxM/UYxS2WyOSBI/AAAAAAAAJJQ/R416Afh-K1I/s000/user.png)
Shirikisho la kandanda duniani,FIFA, limekanusha madai kwamba katibu wao mkuu,Jerome Valcke,alihusika katika kashfa ya ufisadi ambapo hongo ya mamilioni ya dola ilitolewa.
Kashfa hiyo inachunguzwa na Marekani .
FIFA inasema hamna afisa wake yeyote wa ngazi ya juu aliyehusika kwa njia yoyote katika kashfa hiyo.
Inasemekana malipo hayo ya rushwa yalitolewa na serikali ya Afrika Kusini kwa maafisa wa soka wa huko Marekani ili waunge mkono wenzao Waafrika walio ng'ambo katika nchi ya visiwa vya Caribbean.
Waendesha mashtaka wa Marekani wanasema hongo hiyo ilinuiwa kusaidia kununua kura kuiwezesha Afrika Kusini kuwa mwenyeji wa kombe la dunia lililofanyika mwaka 2010.
Subscribe to:
Posts (Atom)